Tuesday 2 September 2014

DAYOSISI YA RUAHA YAPATA MACHEMASI NA MAKASISI WAPYA.
Katika Ibada ya kuwaweka wakfu, iliyofanyika katika kanisa Kuu la Anglikana Iringa, 03/08/2014, takribani mashemasi saba (7) na makasisi (8) waliwekwa wakfu kuhudumia kanisa la Mungu.


Askofu Dr. Joseph Mgomi akiwaweka wakfu machemasi na makasisi

Ibada hiyo iliyoongozwa na Askofu wa sasa Dr. Joseph Mgomi; pia ilihudhuliwa na Askofu Mstaafu wa Dayosisi ya Ruaha Dolnald Leo Mtetemela. Dr. Mgomi aliwaweka wakfu mashemasi 7 ambao ni:-
  1. Alex Malogo
  2. Alfa Kwanga
  3. Bartazar Hepelwa
  4. Yakobo Kilamba
  5. Musa Mtuli
  6. Steve Mbambaga na
  7. Philemon Mfumbe
    Mashemasi wakiwekwa wakfu kwa BWANA


Aidha makasisi 8 waliwekwa wakfu na Askofu Dr. Joseph Mgomi, ambao ni:-
  1. Samson Chadewa
  2. Ernest Ndogwe
  3. Steve Makwaya
  4. Hosea Mlula
  5. Jackson Mhembezi
  6. Simon Meteli
  7. Galus Chuhila na
  8. Brad Galvin

    Makasisi wakiwekwa wakfu kutumika madhabahuni

TheoCentric & Educare inawatakia huduma njema wote mliowekwa wakfu kwa BWANA. Mumjue sana Mungu, na kumtumikia kwa uaminifu Mungu wa Israel. Jilindeni sana nafsi zenu na hilo kanisa; pia mlitoe kwenye matope kanisa la Mungu alilolinunua kwa damu yake mwenyewe. Matendo 20:28.

No comments:

Post a Comment

Welcome